STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 8, 2017

Kibarua cha Bilic West Ham shakani

KAZI anayo. Kibarua cha Meneja wa West Ham United, Slaven Bilic kipo hatarini, ikielezwa ana mechi mbili tu kabla ya kufutwa kazi.
Kwa mujibu wa The Sun, limefichua kuwa kibarua cha Bilic kipo kwenye hatihati kama atashindwa kufanya vema kwenye mechi zijazo za timu hiyo.
Mechi hizo zinahusisha pambano dhidi ya Crystal Palace na Middlesbrough hii ikiwa ni baada ya kupokea kichapo cha aibu cha mabao 5-0 juzi Ijumaa kutoka kwa Manchester City katika pambano la Kombe la FA.
Ushindi wa mechi tatu katika mwezi uliopita, West Ham ilijikwamua toka janga la kushuka daraja, lakini bado imekuwa na muelekeo mbaya kitu kinachowatisha mabosi wa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment