STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 8, 2017

West Bromwich Albion yamkomalia straika wa Napoli

KLABU ya West Brom ipo kwenye mazungumzo ya kutaka kumnyakua straika wa Napoli, Manolo Gabbiadini.
Kwa mujibu wa duru za kimichezo nchini Uingereza zinasema kuwa Albion inazungumza na klabu ya Napioli inayoshiriki Ligi Kuu ya Italia, Serie A ili kumsajili Gabbiadini.
Straika huyo mwenye miaka 25 pia ananyatiwa na klabu za Wolfsburg, Southampton, huku Everton na Stoke City nazi zikitajwa kwenye mbio hizo.
Wolfsburg walikaribia kumnasa Gabbiadini kwa mkono kwa kiasi cha Puni 15 milioni usajili uliopita na Albioni walijaribu kumnasa Agosti mwaka uliopita na sasa inakula sahani moja kumnasa jumla kwenye usajili huu wa Januari.
Gabbiadini aliifungia timu yake bao dhidi ya Sampdoria na kuisaidia kutoka nyuma na kushinda mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment