STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 1, 2013

Bandari yaonja kipigo, Gor Mahia, Sofapaka ziking'ara KPL

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Kenya, Tusker




BAADA ya ushindi mfululizo, vijana wa Bandari Kenya mwishoni mwa wiki waliisherehekea vibaya sikukuu ya Pasaka baada ya kunyukwa na mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Kenya (KPL)  Tusker kwa mabao 2-1, huku Gor Mahia na Sofapaka zikipata ushindi katika mechi zao zilizochezwa jana.
Kipigo ilichopewa Bandari inayochezwa na watanzania wanne waliowahi kutamba na klabu za Simba na Yanga imeipomosha timu hiyo kwa nafasi moja nyuma toka ya tano hadi sita ikizimwa na kasi yake ya kutoa vipigo kwa wapinzani wake baada ya kushinda mara mbili mfululizo na hivyo kusaliwa na pointi zake nane.
Bandari waliokuwa ugenini ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao kwea kuwashtua vijana wa Tom Olaba kocha aliyewahi kuinoa Mtibwa Sugar kwa bao lililofungwa na Eric Okoth kabla ya Jesse Were na Mganda, Andrew Ssekyayomba kuzima matumaini ya Bandari kupata ushindi wa tatu mfululizo.
AFC Leopard wakiwa ugenini walikiona cha mtema kuni siku ya Jumamosi baada ya kunyukwa mabao 2-1 na Muhoroni Youth, huku vijana wa KCB jana walirejea kileleni mwa msimamo baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya mabingwa wa 2010 Ulinzi Stars na kuwaengua Thika United waliokuwa wamekalia kiti hicho kwa saaa 24 baada ya Jumamosi kuicharaza Chemelil 2-1.
Mabao ya vijana hao watunza fedha wa benki ya biashara ya nchini, yaliwekwa kimiani na Jacob Keli na Edward Mwaura na kuifanya timu yao irejee kileleni kwa kujikusanyia pointi 14, mbili zaidi ya Thika.
Nao mabingwa wa zamani wa Kombe la Shirikisho Afrika, Gor Mahia jana ilizinduka katika ligi hiyo kwa kuidonyoa Mathare United kwa bao 1-0 baada ya wiki iliyopita kuzimwa na Ulinzi kwa kulazwa mabao 2-0.
Ushindi huo umeifanya Gor Mahia inayochezwa na kipa wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Ivo Mapunda kukwea hadi nafasi ya 10 ikiwa mbele ya mabingwa watetezi Tusker waliopata ushindi wake wa kwanza katika mechi tatu ilizocheza msimu huu.
Mabingwa wa zamani wa Kenya, Sofapaka nao jana walitoa kipigo kitakatifu kwa Karuturi Sports kwa kuikong'ota mabao 4-2 katika mfululizo wa mechi za ligi hiyo ya Kenya.
Matokeo kamili ya mechi za ligi hiyo ya jirani zilizochezwa mwishoni mwa wiki ni kama ifuatavyo;

Nairobi City Stars v Sony Sugar (2-1)
Thika United v Chemelil (2-1)
Western Stima v Home Boys (1-0)
Muhoroni Youth v Leopards (2-1)
 Tusker  v Bandari (2-1)
KCB v Ulinzi Stars (2-0)





Sofapaka v Kurituri Sports (4-2)






Gor Mahia v Mathare United (1-0)







































No comments:

Post a Comment