STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 1, 2013

Bessa alia wasanii kunyonywa jasho lao


Salim Mbwana 'Bessa' a.k.a Madhira
MCHEKESHAJI Salim Mbwana 'Bessa' amedai kuwa sanaa ya maigizo nchini bado haijanufaisha wadau wake kulingana na ukubwa wa kazi wanayofanya kutokana na kuwapo kwa unyonyaji na wizi unaofanywa na watu wachache waliohodhi soko la fani hiyo.
Bessa ambaye ni mlemavu wa miguu, alisema kwa namna wadau wa sanaa hiyo wanavyochapa kazi, ni wazi kwamba wangekuwa mbali sana kiuchumi akitolea mifano wasanii wa Nigeria.
"Bado sanaa haijaleta mafanikio kama jasho linalovuja kwa wasanii, kuna haja ya  kuongezwa juhudi za kunusuru fani hii ili wadau wanufaike kama wasanii wenzao wa  kimataifa," alisema Bessa anayejiita 'Madhira'.
Alisema hata yeye mwenyewe pamoja na kujivunia umaarufu mkubwa alionao, tangu aanze kuuza sura kwenye filamu na vichekesho mbalimbali, bado hawezi  kutembea kifua mbele kujisifia mafanikio kwani yupo 'choka mbaya'.
"Sanaa haijaninufaisha ipasavyo, sina cha kujivunia kwa vile kuna hali ya ubabaishaji mkubwa kwa wasanii nchini kunyonywa na kuibiwa jasho lao," alisema Bessa.
Mkali huyo aliyewahi kutamba na utunzi wa riwaya katika gazeti hili, kwa sasa ndiye  mtunzi mkuu katika kampuni iliyompa ajira ya kudumu ya ASl Riyamy.

No comments:

Post a Comment