STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 1, 2013

Demba Ba 'awaua' Mashetani Wekundu Darajani


Demba Ba wa Chelsea akiifungia timu yake bao pekee katika pambano la marudiano ya Kombe la FA jioni ya leo

BAO pekee lililofungwa kiufundi jioni ya leo na Demba Ba, lilitosha kuizamisha vinara wa Ligi Kuu ya England, Manchester United katika pambano la marudiano la Robo Fainali ya Kombe la FA dhidi yao na Chelsea.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Stamford Bridge, London lilishuhudiwa hadi wakati wa mapumziko timu zote kiuwa nguvu sawa kwa kutofungana.
Demba Ba alifunga bao hilo lililoipeleka Chelsea hadi fainali ya michuano hiyo alitumbukiza wavuni mbele ya mabeki wa Manchester United katika dakika ya 49.
Manchester walionyesha kulipania pambano hilo, baada ya pambano lao lililochezwa Machi 10 kwenye uwanja wa Old Trafford kumalizika kwa sare ya mabao 2-2, lakini vijana wa darajani waliwakwamisha na kukifanya kikosi hicho cha Sir Alex Ferguson kuelekeza nguvu zake kwenye ligi kuu ili kuambulia taji mwaka huu.
Kwa ushindi huo Chelsea sasa imepata nafasi ya kukwaruzana na Manchester City katika pambano la nusu fainalik, litakalochezwa Aprili 14, siku mpoja baada ya Millwall kuumana na Wigan Athletic.

No comments:

Post a Comment