STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 1, 2013

Irene Paul Hofu filamu ya Kanumba

Irene Paul aliyecheza kama mhusika mkuu katika filamu ya Love & Power

MUIGIZAJI kinara wa filamu ya mwisho ya nyota wa zamani wa fani hiyo nchini, Steven Kanumba iitwayo "Love and Power', Irene Paul amedai anahofia kufufua upya majonzi ya kifo cha Kanumba kilichotokea Aprili mwaka jana.
Irene alinukuliwa wiki hii akisema kutoka kwa filamu hiyo kutaamsha majonzi yake na ya mashabiki wakubwa wa marehemu Kanumba anayetimiza mwaka mmoja  tangu afikwe na mauti ghafla nyumbani kwake Sinza Vatican.
"Kwa kweli sitamani hata kuiona filamu hiyo, naamini itafufua upya majonzi ya  kumpoteza Kanumba ambaye kwangu ni mmoja wa wasanii wakubwa zaidi kuwahi kutokea nchini," alisema  Irene.
Filamu hiyo inatarajiwa kuachiwa rasmi Aprili 12 ikiwahusisha washiriki watatu ambao wametangulia mbele ya haki bila wenyewe kuishuhudia kazi hiyo.
Wasanii hao waliofariki ni Husseni Mkiety 'Sharo Milionea' na John Stephano Maganga waliofariki kwa nyakati tofauti mwishoni mwa mwaka jana.
Kwa mujibu wa taarifa za wasambazaji wa filamu hiyo, inatarajiwa kuzinduliwa rasmi  siku ya kumbukumbu ya kifo cha Kanumba Aprili 6 kabla ya kuingizwa sokoni wiki  inayofuata.
Inaelezwa kuwa simulizi la filamu hiyo linashabihiana na tukio halisi lililosababisha kifo cha Kanumba.

Kava la filamu ya mwisho ya Marehemu Kanumba

No comments:

Post a Comment