STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 1, 2013

Sikinde yachekelea ujio wa Mbinga

Adolph Mbinga (kulia) akicharaza gitaa kando ya Hassan Rehani BItchuka
UONGOZI wa bendi ya muziki wa dansi ya Mlimani Park 'Sikinde' umesema kutua kwa  Adolph Mbinga kumeiongezea nguvu bendi yao ambayo leo inamalizia shamrashamra  za Sikukuu ya Pasaka eneo la Mivinjeni, Dar es Salaam.
Mbinga, nyota wa zamani wa bendi kadhaa ikiwamo African Stars, Mchinga Sound na  Levent Musica, ametua Sikinde wakati bendi hiyo ikimpoteza muimbaji wao nyota,  Athuman Kambi aliyekimbilia Msondo Ngoma.
Katibu Mkuu wa Mlimani, Hamis Mirambo alisema wanaamini kwa uzoefu alionao  Mbinga utaisaidia Sikinde kuzidi kusimama imara na kuwakimbiza wapinzani wao katika  muziki wa dansi.
Mirambo alisema uzuri wa Mbinga mbali na kucharaza magita, pia ni mtunzi na  muimbaji kitu ambacho kitaisaidia Sikinde baada ya kuondokewa na wanamuziki wake  kadhaa wakiwamo waliofariki au kutimkia kwa mahasimu wao Msondo Ngoma.
Mirambo alisema bendi hiyo baada ya kumtambulisha Mbinga mwishoni mwa wiki, leo  watamalizia zoezi hilo katika siku ya Jumatatu ya Pasaka eneo la Mivinjeni, Kurasini.
"Tutamalizia kumtambulisha Mbinga na nyimbo zetu mpya," alisema  Mirambo.

---------

No comments:

Post a Comment