STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 16, 2013

Coastal Union yangang'aniwa mkwakwani


MABINGWA wa zamani wa Tanzania, Coastal Union ya Tanga jioni ya leo imeng'ang'aniwa nyumbani na JKT Ruvu ya Pwani katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani-Tanga.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo MICHARAZO ilipenyezewa hivi punde kutoka Tanga zinasema kuwa timu hizo zimetoshana nguvu kwa kushindwa kufungana katika pambano lililokuwa kali na lenye ushindani.
Kwa matokeo hayo timu hizo zimegawana pointi moja moja na kuifanya Coastal ifikishe pointi 33 na kulingana pointi na Mtibwa Sugar, lakini uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa yanaifanya ikwee nafasi ya tano huku maafande wa JKT wakifikisha pointi 23 na kuchupa kutoka nafasi ya 12 hadi ya 11.
Kipute cha ligi hiyo kinatarajiwa kuendelea tena kesho kwa mechi tatu katika viwanja vya Mkwakwani Tanga kati ya vinara Yanga na wenyeji wao Mgambo JKT, Mtibwa Sugar itakuwa nyumbani kuumana na JKT Oljoro na Toto African itasafiri hadi Kagera kuwakabili wenyeji wao Kagera Sugar kwenye uwanja wa Kaitaba.

No comments:

Post a Comment