STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 16, 2013

Wamorocco watakaoikabili Azam kutua kesho

Kikosi cha As FAR Rabat kinachotarajiwa kuja nchini kesho kuvaana na Azam
Azam wakataowakaribisha Wamorocco kwenye uwanja wa Taifa Jumamosi.
Na Boniface Wambura
WAPINZANI wa Azam katika michuano ya Kombe la Shirikisho, AS FAR Rabat ya Morocco wanatarajiwa kutua nchini kesho (Aprili 17 mwaka huu) saa 7 mchana kwa ndege ya Emirates.
Msafara wa timu hiyo wenye watu 28 utafikia hoteli ya Sapphire iliyoko maeneo ya Kariakoo, Dar es Salaam tayari kwa mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili itakayochezwa Jumamosi (Aprili 20 mwaka huu) saa 10 kamili jioni Uwanja wa Taifa.
Azam na FAR wataumana katikia pambano la raundi ya pili maarufu kama 16 Bora kuwania nafasi ya kutinga hatua ya makundi ya michuano hiyo ya pili kwa ukubwa kwa ngazi za klabu barani Afrika.
Azam iliing'oa BYCII kwa jumla ya mabao 2-1 katika mechi ya raundi ya kwanza awali ikitoa pia Al Nasir Juba ya Sudan Kusini.
Wawakilishi hao pekee wa Tanzania ndiye jicho na roho ya mashabiki wa soka nchini kufuatia wawakilishi wengine wakiwemo Simba na Jamhuri -Pemba kung'olewa mapema kwenye michuano hiyo.
Tayari kikosi cha timu ya Azam ambayo mwishoni mwa wiki waliisimamisha Simba katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kutoka nao sare ya mabao 2-2 imeshaingia kambini kujiandaa na pambano hilo ambalo Azam watahitajika kushinda nyumbani ili kujiweka katika nafasi nzuri kwa mechi ya marudiano ugenini wiki mbili zijazo.
Kwa muda mrefu klabu za kutoka Kaskazini mwa Afrika zimekuwa zikizisumbua timu za Tanzania na Azam wanaoshiriki michuano hiyo ya kimataifa kwa mara ya kwanza wanahitajika kuufuta uteja huo mbele ya Wamorocco hao ambao ni timu ya maafande.

No comments:

Post a Comment