STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 16, 2013


MASHINE ZA UMRI ZAWAUMBUA 'VIJEBA' VYA MICHUANO YA AFRIKA


UDANGANYIFU wa umri wa wachezaji kutoka barani Afrika umekuwa ni jambo la kawaida, lakini teknolojia mpya iliyobuniwa ya kutumia mashine kupima umri sahihi wa wachezaji umeanza kuwaumbua wachezaji 'vijeba' wanaochjachakachua umri ili kujifanya wadogo.
Teknokojia hiyo imewaumbua wachezaji tisa na kuondolewa kwenye michuano ya mataifa  ya Africa chini ya umri wa miaka 17 yanayofanyika nchini Morocco baada kipimo cha kugundua umri kupitia kiganja cha mkono kuonyesha kwamba wana umri mkubwa zaidi kuliko inavyopaswa.
Miongoni mwa wachezaji watatu wanatoka Congo-Brazzaville, Ivory Coast na Nigeria wamefungiwa kabisa kushiriki kwenye mashindano yoyote.
Mashine ya Magnetic Resonance Imaging (MRI) ilitumika kupima viganja vya wachezaji ili kujua ukweli wa umri wao.
Wachezaji ambao wameondolewa kwenye michuano hiyo ni kutoka Congo Cherlevy-Diabala Carim, Hardy Binguila na Bermagin Kangou, kutoka Ivory Coast  ni Dagou Britto, Abdul Diarrassouba na Siriki Dembele, na kutoka Nigeria ni Onyinye Ndidi, Ibrahim Abdullahi and Emmanuel Asadu.
Vikosi vya timu zote tatu vimepunguzwa mpaka kufikia wachezaji 18.
FIFA walianza kufanya utafiti wa umri wa wachezaji kwa kutumia technolojia ya MRI mwaka 2003 lakini wakaanza kuifanyia majaribio machine hiyo kwenye michuano ya U-19 World Cup in Nigeria.
Matokeo ya vipimo kwenye michuano ya kombe la dunia U-17 kuanzia 2003, 2005 na 2007 yalionyesha kwamba asilimia 35 ya wachezaji walikuwa wamezidisha umri unaoruhusiwa.
Wadau wa soka wanatamani kipimo hicho kianze kutumika pia hapa nchini ili kubaini baadhi ya wachezaji 'vibabu' lakini wakijitambulisha wakiwa na umri mdogo, jambo ambalo hata wenyewe wanajishangaa wanavyoongopa.
Credit to shaffihdauda.com

No comments:

Post a Comment