STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 15, 2013

'Mesut Ozil aondoki Santiago Bernabeu'

Mesut Ozil

BABA wa kiungo wa Real Madrid, Mesut Ozil, amesema mwanae hana mpango wa kuondoka Santiago Bernabeu.
Ozil amekuwa akitajwa kutaka kwenda kucheza Ligi Kuu ya England, lakini baba wa mchezaji huyo,  Mustafa amefichua kuwa mwanae hana mpoango huo badala yake anahitaji mkataba mpya wa kuendelea kuitumia timu yake.
Ozil mkubwa alisema mwanae mwenye umri wa miaka 24 ndiyo kwanza amefungua meza ya mazungumzo ya kusalia klabu hapo tofauti na hisia kwamba angependa kumtikia Engaland.
Ozil, nyota wa Kijerumani anatajwa thamani yake ni Pauni Mili 30 na alikuwa akiwindwa na klabu kubwa za Engand, lakini baba yake alisisitiza kuwa; "Mesut anafuraha kubwa ndani ya Madrid," alisema Mustafa na kuongeza imani yao dili mpya kati ya mwanae na klabu yake itambakisha mkali huyo mpaka 2019.

No comments:

Post a Comment