STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 1, 2013

Rais Obama atua salama ardhi ya Tanzania atapa mapokezi ya aina yake

Rais Barack Obama akiburudishwa na ngoma asilia za Tanzania

clip_image001
Add caption
Rais Barack Obama wa Nchini Marekani na Mkewe Michelle Obama wakiwa sambamba na watoto wao, wakiwasili mchana huu kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam mchana huu kwa ziara ya siku mbili hapa nchini.clip_image001[6]Ndege ya Raisi wa Marekani Ikiwa Kwenye Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere, mchana huu.clip_image001[8]Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mgeni wake wa Marekani, Barack Obama aliewasili nchini Mchana huu kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.clip_image001[10]Rais Barack Obama akikagua Gwaride maalum aliloandaliwa akiongozwa na Mkuu wa majeshi ya Ulinzi, Jenelari Davies Mwamunyange.  
RAIS wa Marekani ametua nchini salama na msafara wake ikiwamo familia yake na kupokewa na mapokezi ya aina yake na watanzania wakiongozwa na Rais Jakate Mrisho Kikwete na viongozi wengine waandamizi.
Rais wa Marekani Barack Obama, amewasili katika ardhi ya Tanzania muda mchache uliopita katia kuhitimisha ziara yake barani Afrika.
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete na familia yake pamoja na maafisa wake wa serikali na wacheza ngoma za kitamaduni walimkaribisha Obama na familia yake mjini Dar es Salaam mara aliopowasilia majira ya saa nane mchana.
Mara baada ya ukaguzi wa gwaride na mambo mengine msafara wa Rais huyo anayetokea Afrika Kusini aliambatana na mwenyeji wake kwa ajili ya kuelekea Ikulu ya Tanzania kuendelea na ratiba zake ambapo inaelezwa anatarajiwa kufanyiwa dhifa maalum jioni hii katika makazi ya rais, Ikulu.

No comments:

Post a Comment