STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 1, 2013

Watanzania 60 wakamatwa ziara ya Obama


http://graphics8.nytimes.com/images/2012/11/07/timestopics/Barack-Obama/Barack-Obama-sfSpan.jpg
Rais Obama na familia yake wakiwapungia mikono wananchi
 WAKATI Rais wa Marekani Barack Obama na msafara wake wa watu 600 ukitarajiwa kutua mchana huu nchini Tanzania, Watanzania 60 wanaishi nchini Afrika Kusini wamekamatwa  ikiwa ni maandalizi yaliyokuwa yakifanyika wakati rasi huyo aklipotua nchini humo juzi.ni.

Rais Obama aliwasili Afrika Kusini juzi kwa maandamano akitokea nchini Senegal.

Habari kutoka nchini humo zinasema watu hao 60 walikamatwa baada ya kudaiwa kuishi kinyume cha sheria Afrika Kusini. Baada ya Watanzania hao kutiwa mbaroni na vyombo vya usalama wamehifadhiwa hapa nchini kusubiri  hatua za kisheria zaidi.

Ofisa mmoja wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere, Sadiki Msele amesema Watanzania hao walirejeshwa nchini jana na kwamba hivi sasa wanasubiri sheria kuchukua mkondo wake.

“Safisha safisha kama iliofanyika jijini Dar es Salaam, pia imefanyika Afrika Kusini na kuwaathiri wafanyabiashara na watu wengine,” amesema ofisa huyo.

Hivi sasa Rais Obama yupo njiani kutoka Afrika Kusini akiongoza na mkewe Michelle Obama na watoto wao wawili; Malia na Sasha kwa ajili ya kutua nchini Tanzania  leo kuanzia saa 8 mchana kwa ziara ya siku mbili ambapo moja ya maandalizi yaliyowaacha watu midomo wazi kudekiwa kwa barabara eneo la Ubungo.


Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga ameweka bayana barabnara zitakazofungwa kwa leo na kesho huku akiwataka wananchi wakae umbali wa mita 14 toka barabarani kutokana na hali ya usalama wakati wa ziara ya Obama kokote.
   

No comments:

Post a Comment