STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 1, 2013

Idadi ya wahanga waliolipukiwa mafuta Uganda yaongezeka

http://a57.foxnews.com/global.fncstatic.com/static/managed/img/fn2/feeds/AFP/660/371/photo_1372613034592-1-HD.jpg?ve=1
Muokoaji katika tukio hilo la Uganda akitumia mti kutoa baadhi ya milii ya wahanga wa tukio hilo (Picha:AFP)
IDADI ya watu waliofariki katika ajali ya mlipuko wa moto uliotokana na ajali ya gari la mafuta kuanguka nchini Uganda imeongezeka ikielezwa kuwa sasa imefikia watu 33 badala ya 29 waliotangazwa awali.
Taarifa kutoka nchini humo zinasema baadhi ya majeruhi waliokuwa wamelazwa hospitalini kutokana na kuunguzwa sehemu kubwa ya miili yao wamefariki na kufanya idadi hiyo kuongezeka na kuna hofu idadi ikazidi kutopkana na ukweli wahanga wengi wapo katika hali mbaya licha ya madaktari kupigana kuwaokoa.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi nchini, Andrew Kaweesa alinukuliwa na AFP kuwa mpaka jana walikuwa na takwimu inaoonyesha watu 31 kufariki kutokana na tukio hio na majeruhi wengine 10 wakiwa katika hali mbaya.
Tukio hilo lililotokea mji mkuu wa nchini hiyo, Kampala na iliyohusisha gari ndogo na lori hilo kabla ya kupinduka na watu kukimbilia eneo la tukio kuzoa mafuta na kutokea mlipuko ulioochoma baadhi ya miili kushindwa kutambulika kwa urahisi limetajwa ni tukio kubwa na baya tangu Desemba 2001 ambapo watu 90 walipoteza maisha katika ajali kama hiyo.
Katika ajali hiyo ya juzi, madereva wa bodaboda kadhaa nao walipoteza maisha yao wakati wakikimbilia kuzoa petrol iliyokuwa imebebwa kwenye lori hilo na kamanda Kaweesa alithibitisha pikipiki karibu 20 nazo ziliteketea kwa moto katika ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment