STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 2, 2013

Real Madrid yakaribia kuvunja rekodi ya Uhamisho wa Ronaldo kwa Bale



Cristiano Ronaldo
http://www.standard.co.uk/incoming/article8512730.ece/ALTERNATES/w620/Gareth-Bale-shoots.jpg
Gareth Bale, anayetajwa kuwa bado kidogo tu atue Real Madrid

Madrid, Hispania


KLABU ya Real Madrid inaamini kwamba, sasa ipo hatua za mwisho za kukamilisha uhamisho wa winga wa Tottenham, Gareth Bale baada ya kuanza kujiandaa kutoa pauni milioni 87 ambazo ni sawa na shilingi bilioni 209.3 za Tanzania.



Baada ya wiki nzima Spurs kusisitiza kwamba, Bale hauzwi, sasa Klabu hiyo ya White Hart Lane imenywea na tayari Real inajipanga kutoa dau hilo ambalo litaweka rekodi ya dunia kwa uhamisho wa wachezaji.



Sportsmail limeeleza kuwa linatambua wazi kuwa kikanuni, tayari Spurs imekubali dau hilo, lakini litamthibitisha mchezaji huyo kwa Real Madrid pale tu litakapopata mrithi wake.



Katika kujipanga upya, tayari Spurs inatarajia kukamilisha usajili wa Mshambuliaji wa Valencia, Roberto Soldado kwa dau la pauni milioni 26 (sh. bilioni 62.5 za Tanzania) ambapo pia Kocha Andre Villas-Boas anataka kumng'oa Alvaro Morata katika Uwanja wa Bernabeu ikiwa ni sehemu ya kumwachia Bale.



Morata, 20, anayecheza safu ya ushambuliaji, huku akiwa ameshakifungia mara mbili Kikosi cha Wakubwa cha Real, anatajwa kuwa mmoja wa wachezaji bora kwa siku zijazo.



Spurs inataka kuisisitiza Real Madrid kuwa Morata awe sehemu ya makubaliano ya wao kumwachia Bale.



Morata alikuwa kinara wa ufungaji kwenye michuano ya Ulaya ya wachezaji wenye umri chini ya miaka 21 (Euro U-21), ambayo ilifanyika Israel mwaka huu, baada ya kufunga jumla ya mabao manne na kuiwezesha Hispania kutwaa kombe.



Endapo Spurs itaridhia kumuuza Bale kwa pauni milioni 87, atakuwa amevunja rekodi ya dunia iliyowekwa na Cristiano Ronaldo, aliyetua Real Madrid kwa pauni milioni 80 akitokea Manchester United 2009.



Nyota anayefuata kwa kuuzwa ghali ni Zlatan Ibrahimovic, aliyetua Barcelona 2009, akitokea Inter Milan kwa pauni milioni 56.5. Kaka anafuata kwa pauni milioni 56 kutoka AC Milan kwenda Real Madrid (2009).


Edinson Cavani anashika nafasi ya nne kwa pauni milioni 55, akitokea Napoli kwenda PSG (2013), akifuatiwa na Radamel Falcao, pauni milioni 53, kutoka Atletico Madrid kwenda Monaco (2013).

No comments:

Post a Comment