STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 2, 2013

102 kuiwakilisha JWTZ katika michezo ya EAC


 

WANAMICHEZO 102 kutoka Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) watashiriki katika michezo ya majeshi kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo itafanyika Nairobi, Kenya kuanzia tarehe Jumatatu Agosti 5, 2013 hadi Agosti 17, 2013.

Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania alitarajiwa kukabidhi Bendera ya Taifa kwa wanamichezo hao mchana huu tukio ambalo lilitarajiwa kufanyika bwalo la askari katika kambi ya Twalipo Administration Unit (TAU) iliyopo mkabala na Chuo cha Uhasibu,       Dar es salaam.

Vyombo vya Habari vinakaribishwa kuchukua matukio katika hafla hiyo ya makabidhiano.

Kwa mawasiliano zaidi tel no_0715 270 236, 0754 270 236

Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
                            SLP 9203

Email:ulinzimagazine@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment