STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 1, 2014

Ajali yaua mmoja, yajeruhi 38


AJALI zimeendelea kuua roho za wenzetu baada ya mtu mmoja kufariki na wengine 38 kujeruhiwa baada ya basi la Bunda kugonga kichwa cha treni wilayani Manyoni.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ajali hiyo ilitokea kwenye njia ya makutano na reli na barabara wilayani Manyoni na mashuhuda wakiwemo walionusurika wanadai haraka aliyokuwa nayo dereva wa basi hilo kutaka kuvuka reli ndiyo iliyosababisha ajali hiyo.
Inaelezwa waliojeruhiwa walikimbizwa hospitalini kwa matibabu ambapo wengine walioruhusiwa na wachache wamelazwa kuendelea na matibabu zaidi.

No comments:

Post a Comment