STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 1, 2014

Golden Bush Veterani kuwavaa waliosoma Jitegemee

Golden Bush Veterani
MABINGWA wa soka la maveterani jijini Dar es Salaam, timu ya Golden Bush inayonolewa na nyota wa zamani wa Simba na Yanga, Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio' na Wazir Mahadh 'Mandieta' leo wanatarajiwa kushuka dimba la Kinesi kupepetana na timu inayoundwa na wanasoka waliowahi kusoma Shule ya Sekondari ya Jitegemee JKT.
Kwa mujibu wa Mlezi wa Golden Bush Veterani, Onesmo Waziri 'Ticotico', mechi hiyo inatarajiwa kuchezwa majira ya asubuhi kwenye uwanja huo wa Kinesi uliopo Ubungo, ikiwa ni wiki mpoja tangu walipoichakaza bila huruma Pugu Veterani kwa mabao 8-1 katika mechi ya kirafiki kwenye uwanja huo.
Ticotico, alisema kikosi chao kinachoundwa na wachezaji kama Salum Athuman, Herry Morris, Majuto Komu, Wisdom Ndlovu na wengine waliowahi kutamba kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara na klabu za Simba na Yanga wamejipanga kuhakikisha wanatoa kipigo kingine kwa wapinzani wao watakaoongozwa na Ally Mayay kiungo na nahodha wa zamani wa Yanga.
"Baada ya kuwakunyuga Pugu Veterans goli 8-1, jumamosi (leo) tunatarajiwa kushuka tena kwenye uwanja wa Kinesi maarufu kama St James Park, kuonyeshana kazi na vijana waliosoma Jitegemee wakiongozwa na kocha wao Ally Mayay," alisema Ticotico ambaye pia ni mmoja wa washambuliaji tegemeo wa Golden Bush.

No comments:

Post a Comment