STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 1, 2014

Mtoto wa Rais wa zamani wa Misri anaswa na 'unga'

http://english.ahram.org.eg/Media/News/2012/8/13/2012-634804947670919459-91.jpg
Rais wa zamani wa Misri, Mohammed Mosri
SHIRIKA la habari la Misri linasema kuwa kitinda mimba wa rais aliyeondolewa madarakani, Mohamed Morsi, amekamatwa akishukiwa alikuwa na dawa ya kulevya.
Shirika la habari la taifa linaarifu kuwa polisi walikagua gari walilokuwa na shaka nalo na ndani walimkuta Abdullah Morsi na rafiki.
Inaarifiwa kuwa ndani ya gari piya zilikutikana sigara mbili zilizokuwa na bangi.
Mtoto mwengine wa kiume wa Mohamed Morsi amelaani kukamatwa kwa ndugu yake, na kusema kuwa mdogo wake amesingiziwa tu.
Mohamed Morsi mwenyewe hivi sasa anakabili kesi nne za mashtaka ambayo adhabu yake inaweza kuwa kifo.
BBC

No comments:

Post a Comment