STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 1, 2014

Oljoro JKT yaibana Mbeya City ugenini

Oljoro JKT
Mbeya City iliyobanwa nyumbani
TIMU ya Mbeya City imeshindwa kuendelea kugawa dozi nyumbani baada ya jioni ya leo kulazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya maafande wa Oljoro JKT katika pambano pekee lililochezwa leo kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Licha ya timu zote kushambuliana kusaka mabao hakuna aliyeweza kujipatia bao lolote katika mchezo huo ambao Oljoro wamekiri pambano lilikuwa kali na lililochezeshwa vyema na waamuzi.
Kwa matokeo hayo timu hizo zimegawana pointi moja moja, Mbeya ikifikisha pointi 36 na kuendelea kusalia nafasi ya tatu na Oljoro imefikisha pointi 16 na kusalia nafasi ya 12.
Ligi hiyo intarajiwa kuendelea kesho kwa michezo kadhaa ambapo Simba watakuwa jijini Dar es Salaam kupepetana na Ruvu Shooting pambano linalosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki baada ya timu zote kufungwa katika mechi zao zilizopita.

No comments:

Post a Comment