STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 1, 2014

Chelsea, Newcastle zaua, Arsenal ikifa ugenini

Andre Schurrle
Schurrle akishangilia moja ya mabao yake matatu leo
Stoke City striker Peter Crouch has an attempt during the game against Arsenal
Arsenal walipokuwa ugenini leo
Romelu Lukaku
Lukaku akishangilia bao lake pekee lililoizamisha West Ham

MSHAMBULIAJI kinda wa Chelsea kutoka Ujerumani, Andre Schürrle amefunga hat trick na kuisadia timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 na kuzidi kujichimbia kileleni mwa Ligi Kuu ya England, huku Arsenal ikilala ugenini bao 1-0 mbele ya Stoke City.
Nayo Newcastle ikiwa ugenini iliifumua Hull City kwa mabao 4-1, huku Everton ikiiengua Manchester United katika nafasi ya sita baada ya kuifunga West Ham Utd bao 1-0.
Chelsea inayolewa na Jose Mourinho ikiongozwa na kinda hilo la Ujerumani Schurrle ilipata mabao yake katika kipindi cha pili baada ya dakika 45 za kipindi cha kwanza kumalizika bila timu hizo kufungana.
Schurrle aliianza kuifungia Chelsea bao dakika ya 52 akimalizia kazi nzuri ya Eden Hazard na kuongeza jingine dakika ya 65 akitengenezewa pia na Hazard na kukamilisha hat trick yake dakika ya 69 baada ya Torres kumtengenezea bao hilo.Wenyeji walijipatia bao la kufutia machozi dakika ya  74 kupitia kwa John Heitinga.
Kwa matokeo hayo Chelsea imezidi kujikita kileleni ikifikisha pointi 63, nne zaidi ya Arsenal ambao jioni hii wamegongwa bao 1-0 ugenini na Stoke City kwa mkwaju wa penati iliyofungwa dakika ya 72 na Jonathan Walters baada ya Laurent Koscielny  kuunawa mpira laangoni mwake na mwamuzi Mike Jones kuamuru adhabu hiyo.
Katika mechi nyingine mabao mawili ya Mousa Sissoko na mengine ya Loic Remy na Vurnon Anita  yalitosha kuipa ushindi mnono Newcastle United wa mabao 4-1 dhidi ya wenyeji wao Hull City waliopata bao la kufutia machozi kupitia kwa  Curtis Davies
Everton nayo ilisubiri mpaka dakika ya 81 kujipatia bao pekee lililowapa ushindi nyumbani dhidi ya West Ham United lililofungwa na Romelu Lokaku na kuiengua Manchester United katika nafasi ya sita kwa kufikisha pointi 48 na kuipumia Tottenham Hotspur ye nye pointi 50 itakayocheza kesho.
Pambano la Sunderland dhidi ya West Brom imehairishwa na kwa sasa Liverpool ipo ugenini kuumana na Sputhampton.

No comments:

Post a Comment