STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 15, 2014

Simba kuchaguana Mei 4


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhs3YLOLABWqGLvolfiCNC6htMXFKSuU5hflMOHvDGc2-zA0l2CpuCOvJFrTwrPZkrTmbVZ2p6BZA-J-sqxwf-vQX1ph8hYQpIMmGQDHdD0EDsZA-gzHeTMW9y4K12kU_hCmDn8-mWN7SQ/s1600/simba-logo%255B1%255D.jpg
UCHAGUZI Mkuu wa klabu ya Simba umepangwa kufanyika Mei 4, huku Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo imeteua Kamati Mpya ya Uchaguzi itakayoongozwa na Mwenyekiti Damas Ndumbaro.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Simba, Asha Muhaji Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo ya uchaguzi ni Salum Madenge. Wengine katika Kamati hiyo ni Issa Batenga ambaye ni Katibu, Khalid Kamguna Katibu Msaidizi na Wajumbe Kassim Dewji, Juma Simba na Amin Bakhresa.
na kusisitiza kuwa uchaguzi huo utafanyika Mei 4 na kesho wanachama watakutana kwenye mkutano wa wanachama kwa ajili ya kujadili marekebisho ya katiba ya klabu yao kwa maana ya kuwa na ajenda moja tu tofauti na kilio cha wanachama wengi wa klabu hiyo walioutaka uongozi kuongeza ajenda zaidi.
Mkutano huo utafanyika kesho saa 3 asubuhi kwenye ukumbi wa Officers Police Mass, Oysterbay.

No comments:

Post a Comment