STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 15, 2014

Anelka atimuliwa West Bromwich Albion

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02794/Nicolas_Anelka_2794916k.jpg
KLABU ya West Bromwich Albion ya England imetangaza kumtimua kikiosini nyota wake Nicolas Anelka kwa utovu wa nidhamu. 
Maamuzi ya klabu hiyo yamekuja baada ya Anelka kutangaza kupitia mtandao wa kijamii kuwa ana mpango wa kuondoka klabu hapo.
Anelka amesema kuwa anaondoka baada ya kukosekana muafaka wa tofauti zilizopo kati yake na klabu hiyo kutokana ishara yake yenye utata ambayo inasemekana kuwa ya kibaguzi dhidi ya wayahudi. 
Mshambuluaji huyo mwenye umri wa miaka 35, alipigwa marufuku kutocheza mechi tano na kutozwa faini ya pauni 80,000 na FA, kwa kufanya ishara hiyo ya kinazi, baada ya kufunga bao dhidi ya West Ham United Desemba mwaka jana. 
West Brom imechukua hatua ya kumfuta kazi Anelka kutokana na ishara hiyo na pia kwa sababu ya matamshi yake kwenye mtandao wa kijamii.

No comments:

Post a Comment