STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 15, 2014

Kipre Tchetche bado amganda Amissi Tambwe


Kipre Tchetche wa Azam
Amissi Tambwe (kushoto) akishangilia moja ya mabao yake na Ramadhani Singano 'Messi'
MSHAMBULIAJI nyota wa Azam, Kipre Tchetche ameendelea kumfukuzia Amissi Tambwe katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu, jioni hii akipunguza pengo hadi kufikia mabao saba dhidi ya kinara huyo wa mabao kwenye Ligi Kuu msimu huu aliyefumania mara 19.
Tchetche aliyekuwa mfungaji bora wa msimu uliopita leo amefunga mabao mawili wakati akiiongoza Azam kuitoa nishai Coastal Union kwa kuwalaza mabao 4-0 na kumfanya afikie mabao 12.
Mchezaji huyo kutoka Ivory Coast hata hivyo bado ana kibarua kigumu cha kumfikia Tambwe ambaye kasi yake ya kufumania nyavu imewafanya baadhi ya washambuliaji machachari kusalimu amri katika kukiwania kiatu hicho cha dhahabu.
Miongoni mwa washambuliaji waliokuwa wakifukuzana na Tambwe ni Tchetche raia wa Ivory Coast pekee ambaye amendelea kwenda naye sambamba, huku wazawa kama Elias Maguli wa Ruvu Shooting na Juma Luizio 'Ndanda' wakishindwa kufumania nyavu katika mechi zote za duru la pili mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment