STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 15, 2014

Man City pungufu yaibutua Hull City kwao


MANCHESTER City ikicheza pungufu kwa muda mrefu imefanikiwa kuifyatua Hull City nyumbani kwao kwa kuilaza mabao 2-0 na kurejea kwenye nafasi ya pili ya msimamo wa Ligi Kuu ya England.
Nahodha Vincent Kompany alilimwa kadi nyekundu  dakika 10 ya mchezo kitendo ambacho hata hivyo haikuikatisha tamaa City kwani iliweza kujipatia bao la kuongoza dakika ya 14 kupitia kwa David Silva.
Bao hilo lilidumu hadi wakati wa mapumziko na Hull City kuonekana kukomaa kabla ya kuruhusu bao la ushindi kwa wageni wao lililotumbukiza 'jioni' kabisa ya mchezo huo na Edin Dzeko.
Kwa ushindi huo, City imefanikiwa kutimiza pointi 60 baada ya kucheza mechi 27 na kurejea nafasi ya pili, nyuma ya Chelsea yenye pointi 66 baada ya mechi 29, Liverpool yenyewe imerudi nafasi ya tatu ikiwa na pointi 59 na kesho itakuwa ugenini kumenyana na watani zao Manchester Utd.

No comments:

Post a Comment