STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 15, 2014

Newcastle yadonyolewa, Everton, Stoke zatamba EPL

Ashkan Dejagar akishangilia bao lake pekee lililoipa ushindi Fulham leo
Marko Arnautovic wheels away after putting Stoke ahead
Wachezaji wa Stoke City wakishangilia bao dhidi ya West Ham
Morgan Schneiderlin
Kitu! mchezaji wa Southampton akifunga bao
Juan Cala
Vita ya Evertona dhidi ya Cardiff City
BAO pekee lililofungwa na Muiran, Ashkan Dejagar lilitosha kuiwezesha Fulham kuiangamiza Newcastle United ugenini katika mechi ya Ligi Kuu ya England, huku Everton ikiibuka na ushindi nyumbani wa mabao 2-1 dhidi ya Cardiff City bao la ushindi likipatikana 'jioni'.
Dejagar alifunga bao hilo lililoipa ushindi Fulham katika dakika ya , huku bao lililoibeba Everton dhidi ya Cardiff City likifungwa na 68 dakika tano tu tangu alingia dimbani akitokea benchi akimpokea Dan Burn.
Ushindi huo hata hivyo haujaisaidia Fulham kujitoa mkiani mwa msimamo, ingawa imefufua matumaini ya kuendelea kupambana ili iwemo kwa msimu ujao.
Katika mechi nyingine zilizomalizika hivi punde, Everton ilisubiri dakika za lala salama kuweza kujiandikishia ushindi wa 2-1 nyumbani dhidi ya Cardiff.
Seamus Coleman ndiye aliyefunga bao hilo dakika tatu za nyongezana kuifanya timu yake ilingane pointi na Manchester United ingawa inaendelea kusalia nafasi ya saba.
Everton ilikuwa ya kwanza kupata bao katika dakika 59 kupitia kwa Gerard Deulofeu akimalizia kazi za Osman kabla ya wageni kuchomoa dakika tisa baadaye kupitia kwa Juan Cala na kuonekana kama matokeo yangesalia hivyo yaani timu hizo kufungana bao 1-1 kabla ya Colemans kufunga bao hilo la ushindi.
Nayo timu ya West Bromwich iliyomtimua mshambuliaji wake, Nicolas Anelka ilipata ushindi wa mabao 2-1 ugenini dhidi ya SwanseaCity, huku Sunderland ikilazimishwa suluhu ya bila kufungana nyumbani dhidi ya Crystal Palace.
Nayo timu ya Southampton ikiwa nyumbani ilipata ushindi mnono wa mabao 4-2 dhidi ya Norwich City na Stoke City ikaibamiza West Ham Utd kwa mabao 3-1.
Hivi punde timu ya Aston Villa itakuwa nyumbani kuikaribisha Chelsea inayonolewa na Jose Mourinho ambayo imejizatiti kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment