STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 15, 2014

Sajenti ana nne na Tip Top Connection

KIMWANA aliyejipatia umaarufu katika shindano la Manywele 2007, Husna Idd 'Sajenti', anajiandaa kutoa na filamu nne tofauti chini ya Tip Top Connection anaofanya nao kazi kwa sasa.
Akizungumza na MICHARAZO  kisura huyo aliyewahi kutamba kwenye Miss Tanzania Mkoa wa Singida, alisema filamu hizo zitakuwa zikitoka kwa awamu na ameshirikiana na wakali watupu.
Sajenti alizitaja filamu hizo kuwa ni Adella, Ndoa, Mtawala na Bwege ikiwa ni mwanzo wa 'project' za Tip Top mbali na filamu nyingine alizoshirikishwa na wasanii wenzake.
"Kwa sasa nafanya kazi chini ya Tip Top Connection upande wa filamu na kuna kazi kama nne ambazo zimeshakamilika tayari kwa kuachiwa sokoni kuanzia mwezi huu wa tatu," alisema Sajenti.
Msanii huyo aliyetumbukia kwenye filamu tangu mwaka 2007 baada ya kung'ara kwenye urembo na shindano la Kimwana wa Manywele alisema ndani ya filamu hizo amefanya 'kufuru' na wenzake.
"Sijisifu, lakini ndani ya filamu hizo nimefanya makubwa na wenzangu na mashabiki wasubiri wapate uhondo," alisema kimwana huyo.

No comments:

Post a Comment