STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 22, 2014

Simba waidindia TFF faini ya Sh Mil. 5

KLABU ya Simba imegoma kulipa faini ya sh.milioni 5 kwa shirikisho la soka, TFF, ikiwa ni adhabu kwa mashabiki wake kuvunjam iti katika mechi ambayo haikuwa ikicheza uwanjani.
Simba ilitozwa faini ya sh.milioni 5 baada ya TFF kujiridhisha kuwa wapenzi wa soka waliokaa upande wake kwenye Uwanja wa Taifa wakiwa na fulana nyekundu katika mechi ya kimataifa baina ya Yanga na Al Ahly ya Misri ni wapenzi wa timu hiyo.

Akizungumza jana jijini, Msemaji wa Simba Asha Muhaji alisema timu yake haitolipa adhabu hiyo kwa sababu TFF imeionea na ni kinyume na kanuni zake lenyewe.

Asha alisema kanuni za TFF zinasema "timu mwenyeji ndiyo inayopaswa kubeba dhamana endapo patatokea uharibifu wa mali uwanjani wakati wa mechi."
Alisema mwaka 2012, katika mechi ya Kombe la Shirikisho la klabu za Afrika baina ya Simba na Kiyovu kwenye uwanja huo, mashabiki wa Yanga na wa Simba walifanya uharibifu lakini faini ilililipwa na wao pekee.

TFF iliitoza Yanga jumla ya sh. milioni 20 katika faini na fidia na Simba faini ya sh. milioni 5 katikati ya wiki kutokana na uharibifu wa viti uliofanyika katika pambano la kwanza la raundi ya kwanza ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika mwanzoni mwa mwezi.

Alipulizwa juu ya malalamiko hayo ya Simba jana, Msemaji wa TFF Boniface Wambura alisema timu hiyo haipswi kugomea adhabu hiyo kwa sababu imetolewa baada ya uchunguzi wa kina.

“Tumefanya uchunguzi na kugundua kuwa mashabiki wa Simba na Yanga walishiriki kufanya uharibifu na ndiyo maana tukaamua kuwapiga faini wote.

“Tumetumia ushahidi wa video na kuamua kutuoa adhabu kali kwa klabu ili kukomesha vitendo hivi katika mechi zijazo."

Nipashe

No comments:

Post a Comment