STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 22, 2014

Golden Bush ilivyopepetana na timu ya Wizara ya Afya leo Sinza

Golden Bush Veterani 'Wazee wa Dozi' wakijipanga kabla ya kuanza kwa 'game'
Jamani mnaonaje hawa jamaa tuwapige nane? Golden Bush Veterani
Timu ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakijifua kabla ya kuanza kwa mchezo
Tusipopasha vyema hawa jamaa wanaweza kututia aibu! Afya Fc wakipasha
Mwamuzi Othman Kazi akitetea na mchezaji wa Wizara ya Afya
Waambie wenzenu mjipange hawa jamaa wanapiga nyingi ooh! Refa Kazi akiagana na mchezaji wa Afya FC
 
Kipa wa Golden Bush, Machota akidaka mpiga ulioelekezwa langoni mwake na Afya FC
Hapa kazi tu, msitutanie nyie!
Said Kokoo akipitwa na mchezaji wa Afya Fc huku wachezaji wenzake wakitafakari namna ya kuupata mpira
Wisdom Ndhlovu wa Golden Bush akiuwahi mpira karibu na lango lake
Chupuchupu Golden Bush watunguliwe baada ya mpira wa kona kutoka nje
 

Said Kokoo (26) akitafuta mbinu za kumnyang'anya mpira Ally wa timu ya Wizara ya Afya
Beki wa pembeni wa Golden Bush, Majaliwa akimiliki mpira huku akinyemelewa na mchezaji wa Afya FC
Mimi ndiyo Majaliwa Mwaigaga bana!
Kama Ronaldo vile!
Wazir Mahadh (10) akionyesha vitu vyake

Shomari (9) wa Golden Bush aliyefunga bao pekee la mchezo baina yao na timu ya Wizara ya Afya akichuana kuwania mpira
Sijui nimtoke vipi? Mchezaji wa Afya Fc akitafakari mbele ya Majaliwa
Mchezaji wa Afya Fc Ally akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Golden Bush
 
 
Patashikla langoni mwa Golden Bush
Kipa Machota akionyesha ujuzi wake, huku akifuatwa na mchezaji wa Afya na Majaliwa (17) anayecheza wote timu ya Golden Bush akiwa tayari kutoa msaada
Bonge la 'Mido' Makocha Mayay wa Golden Bush akionyesha 'maujuzi' yake
 

Saidi Kokoo akimtoka mchezaji wa Afya Fc
Peke yetu jamani tutulie, Mandieta, Kokoo na Ticotico wa Golden Bush
Heka heka langoni mwa Golden Bush
Tupozeni makoo tukawafanyie wapinzani! Wachezaji wa Golden Bush wakiwa mapumziko
Dah! Hivi tulikuwa tunacheza na Simba, Yanga au Golden Bush Afya Fc wakiwa wamepumzika
Kocha wa timu ya Afya, Wille (kulia) akiongea na wachezaji wake wakati wa mapumziko
Jamani mbona mnawachelewesha? Kocha Madaraka Suleiman 'Mzee wa Kiminyio' (kushoto) akiongea na wachezaji wake wa Golden Bush huku Herry Morris naye akiwa pembeni ( aliyesimama jezi ya njano) 
 

Makocha Herry Morris na Madaraka Seleman wakitetea na wachezaji wao
Jamani hili jua la leo kama kiama! Marefa wa pambano hilo wakitetea wakati wa mapumziko.
Hekaheka langoni mwa timu ya Afya Fc
Salum Swedi 'Kussi' akionyesha makali yake
Oyaa jikaze mtoto wa kiume! Kipa wa Afya akiwa chini baada ya kuumia huku mwamuzi Othman Kazi akimjulia hali
Kazi imeisha! Othman Kazi akitoka uwanjani baada ya kumaliza pambano la Golden Bush Veterani dhidi ya timu ya Wizara ya Afya ambapo Golden walishinda bao 1-0.

No comments:

Post a Comment