STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 10, 2014

Danny Lyanga ajinadi Simba na Yanga

Danny Lyanga (kulia) akikokota mpira katika mechi ya Ligi Kuu
MSHAMBULIAJI nyota wa Coastal Union, Danny Lyanga amesema yupo tayari kutua katika klabu za Simba, Yanga au Azam iwapo zitakuwa zimevutiwa na kumhitaji kuzichezea kwani yeye 'habagui'.
Mfungaji Bora huyo wa Coastal kwa msimu uliopita alipofunga mabao saba, anasema soka ndiyo kila kitu kwake hivyo hana jeuri ya kuchagua timu ya kuichezea kama itamvutia kimasilahi.
Lyanga ambaye alikuwa miongoni mwa wachezaji walioirejesha Coastal kwenye Ligi Kuu misimu miwili iliyopita, alisema wapo baadhi ya watu huwatia hofu wachezaji kujiunga na klabu kubwa.
Lakini kwake yeye hawezi kutishwa na hofu ya kuuliwa kipaji chake kwa kujiunga na timu hizo kubwa kwa madai anajiamini uwezo mkubwa alionao katika kusakata kandanda.
"Kokote nipo tayari kucheza, ninachoangalia ni masilahi kwa vile soka la sasa ni ajira, hivyo wachezaji hatupaswi kuchagua timu za kuzichezea kwa kisingizio cha mapenzi kwani ni kujitia umaskini."
Lyanga alisema na kuongeza, kuendekeza mapenzi katika soka ndicho kilichosababisha baadhi ya mastaa wa zamani kufa maskini kwa kuhofia kuhamia kwingine hata kama kuna masilahi zaidi.
"Siangalii timu kwangu masilahi kwanza kwa vile maisha yangu ya baadaye yapo mikononi mwangu mwenyewe, nikizembea kidogo inaweza kula kwangu na hatimaye kuja kuchekwa," anasema.
Kumekuwa na dhana mbaya kwa baadhi ya mashabiki na wachezaji wakitishika wachezaji chupukizi kujiunga na klabu kubwa wakiamini wataua vipaji vyao, ingawa hakuna ukweli wowote.

No comments:

Post a Comment