STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 10, 2014

Muumin airejesha tena Double M Sound

* Alihama jiji kujichimbia Kahama
* Ambeba Ally Akida 'Tetenasi'
Mwinjuma Muumin 'Kocha wa Dunia' akizungumza leo jijini Dar
"Siyo lazima watu wote tuwe Dar, tutakuwa tunakuja kurekodi au kufanya maonyesho Dar lakini kwetu Kahamaaaa"
Waimbaji mpya wa Double M Sound, Furaha Mkwama na Vampire wakiwapa vionjo wanahabari (hawapo pichani)
Furaha (kushoto) achana naye ana sauti siyo mchezo...!
Muimbaji mwingine mpya, Shazi (kulia) akitoa vionjo huku akiangaliwa na Vampire, Muumin na Drumer Boy, Chocholii
Shazii akiendelea kuonyesha maujuzi yake
Muumin akifafanua jambo
Vampire
Sehemu ya kikosi kipya cha Double M Sound wakishoo baada ya mkutano wa pamoja
Vampire
Chocholii
Chocholii na Queen Vero unamkumbuka mnenguaji huyu...naye ndani ya nyuma
Furaha Mkwama katika pozi, mdada huyu nouma kwa sauti
Siyo sauti tu, bali hata mvuto wa sura na umbo hajamboo!
Mimi ndiye Chocholii Machine a.k.a Drumer Boy
NYOTA wa muziki dansi nchini, Mwinjuma Muumin 'Prince' a.k.a Kocha wa Dunia ametangaza rasmi kuirejesha bendi yake ya zamani ya Double M Sound 'Wana Mshikemshike' lakini wakilihama jiji la Dar es Salaam na kutua mjini Kahama, mkoani Shinyanga.
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Muumin alisema ameamua kwenda kujichimbia Kahama, baada ya kubaini mjini huko ndiko penye mafao ya kutosha na mahali pa kurejesha heshima mjini baada ya kitambo kirefu cha ukimya wake.
Muumin anayefahamika pia kama Mzee wa Chelsea, alisema bendi yake hiyo mpya itaundwa na wanamuziki 14 na mafundi mitambo wawili ambao baadhi ya wanamuziki hao  walitambulishwa kwa wanahabari katika mkutano huo uliofanyika ukumbi wa Vijana Social.
"Baada ya kutafakari kwa kina na hasa baada ya kupokewa vyema na wakazi wa Shinyanga, nimeamua kuirejesha Double M Sound na tunatarajia kuondoka asubuhi ya kesho kwenda kuweka makazi ya kudumu tukiwa tumekamilika," alisema.
Alisema wataanza kuwasha moto kuelekea kwenye sikukuu ya Pasaka kwa kufanya onyesho lao la kwanza April 18 katika ukumbi wa The Dreams, uliopo Kakola machimboni Kahama kabla ya kuelekea Ngara kuwasha moto siku inayofuata kwenye ukumbi wa City Center.
"Baada ya hapo siku ya Pasaka tutakuwa ukumbi wa Manispaa huko Kibondo mkoani Kigoma na kumaliza burudani yetu siku ya Jumatatu ya Pasaka, FM Hall, Kasulu na kurejea Kahama kujifua kwa mazoezi kabla ya kuingia studio kurekodi nyimbo zetu za kwanza," alisema.
Muumini alisema Double M itazitumia nyimbo zote za zamani na zile mpya ambazo amezitunga na kuziimba katika bendi mbalimbali wakati wakijipata kutoa kazi mpya na kudai kitu kipya cha kuanzia kitakuwa 'Utafiti wa Mapenzi'.
Muumin alisema hakuona haja ya kutafuta jina jipya katika ujio wake mpya wakati Doun]ble M Sound ilikuwapo na ilijijengea jina kubwa kabla ya kuzimika baada ya uzinduzi wa albamu ytake ya 'Titanic'.
Juu ya kikosi chake, Muumin alisema kwenye safu ya uimbaji yupo yeye mwenyewe kama nahodha akisaidiana na Richard Magige, Sherri 'Shazi' Abubakar na wadada Furaha Mkwama na Nana Mwashauya 'Vampire'.
"Kwenye solo yupo Ally Akida 'Tetenasi' ambaye pia hupiga Rhythm atakalosaidiana na David Shidodo ambaye pia hupiga besi kumsaidia mcharaza gitaa hilo zito, Said Bell, huku mpapasa kinanda ni Pascal Kiinuka na tumba yupo Husseni Ngalawa na drum kuna Chocholii Machine.

No comments:

Post a Comment