STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 10, 2014

Tanzania yazidi kuporomoka FIFA

Taifa Stars
LICHA ya kuambulia sare ya 1-1 ugenini na Namibia mwezi uliopita, Tanzania imezidi kuporomoka kwenye orodha ya viwango vya soka vya FIFA baada ya kushuka kwa nafasi tano toka nafasi yake ya awali.
Baada ya kuteleza kwa nafasi moja mwezi uliopita, Tanzania imeanguka tena kwa nafasi tano na kukamata nafasi ya 122 katika viwango vya soka vya dunia vya kila mwezi vilivyotolewa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) jana.
Tanzania iliyotoka sare ya bao 1-1 ugenini katika mechi iliyopita ya kirafiki dhidi ya Tunisia, sasa inakamata nafasi ya 37 barani Afrika huku ikishika nafasi ya tatu Afrika Mashariki na Kati, na nafasi ya nne katika Ukanda wa Cecafa wa Afrika Mashariki na Kati.
Hispania imeendelea kuongoza 10 bora ikifuatwa na Ujerumani, Ureno, Colombia, Uruguay, Argentina, Brazil, Uswisi, Italia na Ugiriki.
10 bora barani Afrika inaongozwa na Ivory Coast iliyoko nafasi ya 21 duniani ikifuatwa na Misri (24), Algeria (25), Ghana (38), Cape Verde (42), Nigeria (45), Tunisia (49), Cameroon (50), Guinea (51) Mali inayokamata nafasi ya 59 duniani.
Uganda iliyoshuka kwa nafasi moja, bado inaongoza Ukanda wa Cecafa ikiwa nafasi ya 18 Afrika na 86 duniani, ikinyemelewa na Ethiopia (27 Afrika, 101 duniani), Kenya (29/106), Sudan (33/117), Tanzania, Burundi (38/125), Rwanda (39/129), Shelisheli (48/177), Eritrea (51/200), Sudan Kusini (52/201), Somalia (53/202) na Djibout inayofunga pazia Afrika ikiwa nafasi ya 204 duniani.

No comments:

Post a Comment