STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 10, 2014

Man U yafa Ujerumani, Barce aibu tupu kwa Atletico Madrid

Franck Ribery akipiga shuti langoni mwa Manchester United
Bayern Munich
Oyooo bayern Munich wakishangilia ushindi wao dhidi ya Mashetani wekundu ambao wachezaji wake (kushoto) wakiwa katika simanzi
Neymar akiipigania Barcelona mbele ya wachezaji wa Atletico Madrid
Koke scores for Atletico Madrid v Barcelona
Koke akiifungia Atletico bao pekee
BAO pekee lilifungwa katika dakika tano na Koke lilitosha kuitoa nishai Barcelona katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na kuivusha Atletico Madrid katika Nusu Fainali ya michuano hiyo huku Manchester United ikishindiliwa mabao 3-1 na Bayern Munich na kung'olewa michuanoni.
Koke alifunga bao hilo akimalizia krosi ya Adrian na kuwafanya vinara wa Ligi ya Hispania kuiondosha Barcelona kwa jumla ya mabao 2-1 baada ya mechi ya awali kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
Atletico sasa inaungana na timu za Real Madrid, Chelsea na Bayern Munich iliyoifumua Manchester United kwa mabao 3-1 na sasa wanasubiri droo ya kujua nani atacheza na nani katika hatua hiyo.
Katika mechi ya mjini Munich, Ujerumani wenyeji na mabingwa watetezi wa michuano hiyo walikunjua makucha yao kwa Mashetani Wekundu kwa kuifumua mabao 3-1, baada ya mechi yao ya awali kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
United ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 57, mfungaji beki wake Mfaransa, Patrice Evra aliyefumua shuti kali kwa guu la kushoto baada ya kupokea pasi ya Antonio Valencia.
Hata hivyo wenyeji walilisawazisha bao hilo sekunde 22 baadaye kupitia kwa Mario Mandzukic baada ya kutumia fursa ya wachezaji wa United kufurahia bao lao.
Thomas Muller aliifungia  Bavarian bao la pili dakika ya 68 kwa pasi ya Arjen Robben ambaye katika mchezo wa jana aliisumbua ngome ya Mashetani kabla ya kufunga mwenyewe katika dakika ya 76 na kuzima ndoto za vijana wa David Moyes kufanya maajabu kwenye michuano hiyo ya Ulaya.

No comments:

Post a Comment