STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 10, 2014

Ramsey kuivaa Wigan FA Cup

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/01738/aaron_ramsey_1738865c.jpg
MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha kuwa Aaron Ramsey yuko tayari kuanza katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la FA dhidi ya Wigan Athletic Jumamosi. 
Kiungo amekuwa nje ya uwanja toka Desemba 26 mwaka jana kutokana na majeraha ya msuli lakini aliingia kama mchezaji wa akiba katika kipindi cha pili kwenye mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Everton Jumapili iliyopita.
Wakati huohuo, Mesut Ozil na Laurent Koscielny wote hawatakuwepo katika mchezo huo utakaochezwa Wembley wakati Kieran Gibbs, Tomas Rosicky na Alex Oxlade Chamberlain nao wakiwa katika hatihati ya kuukosa mchezo huo kutokana na majeruhi. 
Wenger amesema Ramsey yuko tayari kuanza katika mchezo dhidi ya Wigan lakini ana wasiwasi na Gibbs, Rosicky na Oxlade-Chamberlain kama watakuwa tayari kwa ajili ya mchezo huo. 
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa anategemea kila mchezaji atatoa mchango wake kwasababu wana uzoefu wa kutosha na wamecheza mechi kubwa zaidi ya hiyo katika michuano ya FA.

No comments:

Post a Comment