STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 18, 2014

DIEGO COSTA AJIFUNGA MITANO DARAJANI

MSHAMBULIAJI wa Atletico Madrid, Diego Costa amekamilisha usajili wa kujiunga na Chelsea kwa kusaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo ya London.
Ada ya uhamisho ya mshambuliaji huyo inaaminika kuwa ni paundi milioni 32.
"Nina furaha sana kujiunga na Chelsea," alisema Costa. "Kila mmoja anafahamu kwamba hii ni klabu kubwa katika ligi ya ushindani mkubwa na nina furaha sana kuanza maisha mapya nchini England."
Costa anakuwa mchezaji wa tatu kutua Chelsea kufuatia kusajiliwa kwa Cesc Fabregas kutoka Barcelona na Mario Pasalic (19) kutoka klabu ya Croatia ya Hajduk Split.
Mshambuliaji huyo alifunga magoli 36 katika mechi 52 alizochezea Atletico Madrid msimu uliopita ambao walitwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania kwa mara ya kwanza tangu 1996 na walifika hatua ya fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
BBC

No comments:

Post a Comment