STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 18, 2014

Jose Mourinho amchokonoa Wenger kuhusu Sami Khedira

Sami Khedira
KLABU ya Chelsea imepata nguvu mpya ya mapambano ya kupata saini ya Sami Khedira kufuatia wakala wake kudai kuwa hakuna mazungumzo yoyote yaliyofikiwa mpaka sasa na Arsenal.
Meneja wa 'The Blues' Jose Mourinho amefanikisha usajili wa mlinzi wa kushoto Filipe Luis akitokea Atletico Madrid kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £18 na sasa anajipanga kwa ajili ya kiungo wa kimataifa wa Ujerumani Khedira.
Hapo kabla ilikuwa imefahamika kuwa Arsenal imekamilisha dili la uhamisho wa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 kwa ada ya pauni milioni £20, lakini walikwama kufikia makubaliano ya mshahara wake wa wiki ambao nyota huyo alikuwa akitaka zaidi ya pauni £180,000.
Amekaririwa wakala wa Khedira, Jorg Neubauer akisema 
 ‘Hatuko kwenye mazungumzo na Arsenal. Sidhani kama ada itakubalika, vinginevyo wange kwisha kunipatia taarifa.’
Khedira amekuwa akimpendeza Mourinho tangu wakati huo akiwa bosi wa Real na inaelezwa kuwa huenda Mourinho akamvuta Stamford Bridge.
Recruit: Chelsea boss Jose Mourinho has already acquired Diego Costa and Filipe Luis
Usajili: Bosi wa Chelsea Jose Mourinho amesha msajili Diego Costa na Filipe Luis

Wakati hayo yakiwa hivyo, Chelsea imethibitisha makubaliano na mlinzi wa kushoto wa Atletico Fillipe Luis.
Mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 28 atakamilisha uhamisho wake baada ya kufanikisha kipimo cha afya na makubaliano ya maslahi binafsi.
Usajili wa Mourinho unaendelea akiwa bado katika ushawishi kwa Khedira, matumaini yake ya kumsajili Antoine Griezmann aliyethaminishwa kwa pauni £20 na klabu yake ya Real Sociedad huenda yakagonga mwamba kufuatia upinzani mkubwa kutoka kwa vilabu vya Monaco na Liverpool.
Blue: Chelsea have confirmed the signing of Brazilian defender Filipe Luis (left)
Chelsea imethibitisha kumsajili mlinzi wa kibrazil Filipe Luis

No comments:

Post a Comment