STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 18, 2014

Ze Gunners wazidi kujiimarisha England

Striking a pose: Debuchy said he was excited to be playing Champions League football again
KLABU ya Arsenal imezidi kujiimarisha kwa kumsajili beki wa kulia wa Ufaransa, Mathieu Debuchy kutokea klabu ya Newcastle United.
Debuchy, 28, amesajiliwa kwa nia ya kuziba pengo la beki wa kulia, Mfaransa mwenzake, Bacary Sagna aliyetimka Emirates na kujiunga na mabingwa wa Ligi Kuu, Manchester City majira haya ya kiangazi mwaka huu.
Debuchy alijivunia usajili huo na akasisitiza kuwa umuhimu wa ligi ya mabingwa ndio kichocheo cha yeye kujiunga na Asernal.
“Najivunia kujiunga na klabu kubwa kama hii na kuvaa rangi zake, ni moja ya klabu kubwa zaidi duniani,” beki huyo wa kulia aliuambia mtandao wa Asernal.com.
“Naangalia mbele nikiwa na Aserne Wenger na kuisaidia timu kuendeleza mafanikio ya msimu uliopita ya kutwaa kombe la FA”.
“Kucheza tena ligi ya mabingwa ni furaha kubwa kwangu na nitajitahidi kadri ya uwezo wangu kuisaidia Asernal kushindania kombe”
Debuchy amewasili  Arsenal kurithi mikoba ya Bacary Sagna ambaye hakuonesha kiwango kikubwa katika fainali za Kombe la Dunia akiwa na Ufaransa.
Kutua kwa mcjhezaji huyo kumekuja siku chache baada ya kumnasa mshambuliaji nyota wa Barcelona, Alexis Sanchez kutoka Chile.

No comments:

Post a Comment