STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 3, 2014

Tip Top Connection, TMK Wanaume wakumbushia Chama Kubwa

http://www.timesfm.co.tz/content/uploads/2014/7/10/cache/ww_full.JPG
Wakurugenzi wa makundi ya Top Top na TMK Wanaume Family, Said Fella na Babu Tale
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEji03SsvzTETvUSLX83T9Hg7KAhg3k3Q-EnQ9WOjWg-mhWbbEtjsrKzinlaFzWotAvkq_qOaxwJiGHuOv2i6p1BVJf7AKY7CUUrESwrzZK4bnTQZW_GWhAYo2rBp02Mnw0GKOigVxglqtg/s400/19.JPG
Baadhi ya vichwa vya Tip Top
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhqIjwnLbpME9u1DjM5-e6u8k893BW186Gkejj3lQqLtuoBZp7DINoSYUtldaQIK7pgzbyKZuQQ5m3iFQ8Iqd4kBZq6_BUF4IeAXoSW3up9yRvGKVkXU8dvhrL5WNcTpSsbAS5WAw7IxvQ/s640/b2b31624f03011e29c2822000a1fbe4c_7.jpg
Majembe ya TMK Wanaume Family
MAKUNDI maarufu ya muziki wa kizazi kipya nchini, Tip Top Connection na TMK Wanaume Family wameungana tena na kurekodi kati ya pamoja wakikumbushia enzi za kibao chao cha 'Chama Kubwa'.
Makundi hayo yanayoongozwa na wadau wakubwa wa muziki nchini Said Fella 'Mkubwa' na Hamis Tale 'Babu Tale' yamerekodi wimbo huo katika studio za Barning Records, japo mpaka sasa bado hawajaupa jina mpaka kwanza wajadiliane kuutafuta jina muafaka.
Akizungumza na MICHARAZO, mmoja wa wasanii wanaounda makundi hayo, Madee alisema wimbo huo unatarajiwa kuachiwa hewani mara baada ya kutungiwa jina na ni moja ya wimbo bomba.
"Baada ya kitamboi kirefu tangu tutoe Chama Kubwa, Tip Top Connection na TMK Wanaume Family tumeungana tena na kufyatua wimbo wa pamoja ambao bado hatujaupa jina mpaka sasa," alisema Madee.
Madee alisema wimbo huo umewashirikisha wasanii wa makundi hayo yote akiwamo yeye mwenyewe (Madee), Tundaman, Dogo Janja, Chege, Mheshimiwa Temba.
Msanii huyo aliongeza mara baada ya wimbo huo kuanza kurushwa hewani wataanza mchakato wa kurekodi video ya wimbo huo.

No comments:

Post a Comment