STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 3, 2014

Kilichomponza Lukaku Chelsea hadharani

http://i1.liverpoolecho.co.uk/incoming/article6554287.ece/alternates/s615b/3366398.jpg
LICHA ya Romelu Lukaku kuwa mfungaji mzuri, mwenye kasi na umri mdogo wa miaka 21 tu, kocha Jose Mourinho alipoteza mapenzi dhidi yake saa 72 tu baada ya kukosa penalti wakati wa kupigiana "matuta" katika fainali ya European Super Cup dhidi ya Bayern Munich Septemba mwaka jana.
Kisha Desemba mwaka jana Mourinho akasema: "Romelu Lukaku anapenda kuongea. Ni kijana mdogo anayependa sana kuongea. Lakini jambo ambalo halisemi ni kwa nini ameenda Everton kwa mkopo.
"Hilo ndilo jambo pekee ambalo hasemi. Na mara ya mwisho nilipowasiliana naye nilimwambia hilo hilo. Ni jambo ambalo alipaswa kulisema, sababu kwanini hayuko na Chelsea na yuko Everton."
Lukaku ameuzwa rasmi kwa Everton kwa paundi milioni 28, ada ya uhamisho ambayo imevunja rekodi ya klabu hiyo iliyokuwa ikishikiliwa na Mbelgiji mwenzake Marouane Fellaini aliyenunuliwa kwa paundi milioni 15, na amesaini mkataba wa miaka mitano.

No comments:

Post a Comment