STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 1, 2014

Chelsea, Arsenal, Southampton zaua England

Arsenal's Alexis Sanchez celebrates
Sanchez akishangilia moja ya mabao yake mawili leo
Oscar celebrates scoring for Chelsea against QPR
Oscar akiifungia Chelsea bao la kwanza
Victor Wanyama
Wanyama akiwa na wachezaji wenzake wakishangilia bao lake pekee la mapema lililotokana na shuti kali la umbali kama mita 40 na kuipa Soputhampton ushindi wa bao1-0 ugenini
VINARA wa Ligi Kuu ya England imezidi kujiimarisha kileleni mwa ligi hiyo baada ya kuizamisha QPR kwa mabao 2-1 na Arsenal kuifanyia mauaji Burnley kwa kuinyuka mabao 3-0.
Chelsea ikiwa uwanja wa nyumbani wa Stanford Bridge ilipata mabao yake kupitia kwa Oscar dakika ya 32 na mkwaju wa penati ya dakika ya 75 kupitia Eden Hazard na bao la wageni lilifungwa na Carlie Austin. Ushindi huo umeifanya Chelsea kufikisha mechi ya 10 ila kupoteza katika ligi hiyo.
Katika mechi nyingine Arsenal ilipata ushindi nyumbani wa mabao 3-0 dhidi ya Burnley kupitia mabao mawili ya Alexis Sanchez na jingine la Alex Oxlade-Chamberlain.
Nayo timu ya Southampton imeendeleza wimbi lake la ushindi na kuifukuza Chelsea ikiwa nafasi ya pili baada ya kupata ushindi ugenini dhidi ya Hully City bao pekee likifungwa na Vincent Wanyama.
Everton ikiwa nyumbani iling'ang'aniwa na Swansea City na kutoka suluhu bila ya kufungana, huku West Brom wakipata ushindi mwembemba ugenini wa bao 1-0 dhidi ya Leicester City, huku West Ham United ikiwa ugenini ililazlmisha sare ya 2-2 dhidi ya Stoke City.

No comments:

Post a Comment