STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 1, 2014

Newcastle yaendeleza maajabu, yaizamisha Liverpool


Mario Balotelli akichezwa vibaya na mchezaji wa Newcastle Un ited leo
BAO pekee lililowekwa kimiani na Ayonze Perez limeifanya Newcastle United kuendeleza maajabu baada ya jioni ya leo kuilaza Liverpool bao 1-0.
Perez alifunga bao hilo dakika ya 73 na kuifanya timu hiyo ya Newcastle imepata ushindi wa tatu mfululizo baada ya kuinyuka Spurs na kisha kuivua taji la Capital One League, Manchester City.
Kipigo hicho kimezidi kuiweka pabaya Liverpool ambayo imeshindwa kuonyesha makali yake kama ilivyokuwa msimu uliopita ilipoonekana kama ingetwaa taji la Ligi ya England kabla ya kuzidiwa na Man City.

No comments:

Post a Comment