STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 1, 2014

Real Madrid yapiga mtu 4-0, Atletico yatakata pia

Karim Benzema
Benzema akiwajibika
Real Madrid
Ronaldo akipongezwa na wenzake
CHRISTIANO Ronaldo ameendeleza rekodi yake ya mabao baada ya usiku huu kuifungia timu yake ya Real Madrid bao moja wakati wakipata ushindi wa mabao 4-0 ugenini dhidi ya Granada.
Ronaldo alifunga bao lake la 17 katika mechi 10 na kutimiza mabao 23 katika mechi 12 za michuano yote ya msimu huu mpaka sasa 9 katika dakika ya pili ya mchezo kabla ya James Rodriguez kufunga mengine mawili na Karim Benzema kumaliza udhia na kuipa madrid ushindi huo mnono.
Majirani na wapinzani wa jadi wa Real, Atletico Madrid wakiwa nyumbani walipata ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Cordoba.
Mabao ya washindi yalifungwa na Delgado Pacheco aliyejifunga dakika ya 43 kabla ya wageni kusawazisha kupitia kwa Ghilas dakika ya 53 na Griezmann kuongezea wenyeji bao dakika tano baadaye na Mario Mandzukic kufunga bao la tatu na Raul Garcia kuhitimisha bao la nne kabla ya Ghilas kufunga bao la pili la Cordoba.
Hivi Barcelona wapo uwanja wa nyumbani kuumana na Celta Virgo na matokeo bao 0-0.

No comments:

Post a Comment