STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 1, 2014

Kiemba, Chanongo wakacha 'Kitimoto' Msimbazi, Kisiga naye...!

Kiemba akichuana na Coutinho wakatia wa pambano la Simba na Yanga hivi karibuni
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2014/10/46.png
Haruna Chanongo (kushoto)
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2014/07/IMG_9835.jpg
Shabaan Kisiga
WACHEZAJI Amri Kiemba na Haroun Chanongo wameshindwa kutokea kwenye kikao cha Kamati ya Nidhamu ya Simba SC kilichokua kifanyike jana ili kujitetea kutokana na kupewa adhabu ya kusimamishwa kusikojulikana huku wakiwa hawataoa udhuru wowote kama Shaaban Kisiga waliyesimamiwa naye.
Rais wa Simba SC, Evans Elieza Aveva alisema kuwa Kiemba na Chanongo hawakutokea licha ya kutakiwa kufanya hivyo na wala hawajatoa taarifa yoyote, huku Kisiga akitoa udhuru.
“Tuliwaagiza wafike makao makuu ya klabu Saa 4:00 asubuhi (jana), lakini hadi saa 6:00 mchana walikuwa hawajafika na hawakutoa taarifa yoyote, kwa hivyo ikabidi Wajumbe wa Kamati ya Nidhamu watawanyike,”alisema.
Hata hivyo, Aveva alisema baadaye Kisiga alipiga simu kujieleza kwamba amekwama kwenye foleni na waakamuambia hana sababu ya kufika tena, kwa sababu kikao kimeahirishwa.
Alipoulizwa ni hatua gani watachukuliwa wachezaji hao, Aveva alisema; “Kwanza Kamati ya Nidhamu ilete ripoti ya maandishi kwa Kamati ya Utendaji juu ya kikao chao, baada ya hapo Kamati ya Utendaji itatoa uamuzi,”alisema.
Watatu hao, Shaaban Kisiga ‘Malone’, Amri Kiemba na Haroun Chanongo waliondolewa kwenye kambi ya Simba SC mapema wiki hii kwa sababu mbalimbali.
Kisiga alirejeshwa Dar es Salaam kutoka Mbeya kwa tuhuma za kutoa majibu ya kifedhuli kwa uongozi kabla ya mchezo na Prisons Jumamosi, wakati Kiemba na Chanongo wanatuhumiwa kucheza kwa kiwango cha chini.

No comments:

Post a Comment