STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 1, 2014

Rasmi sasa! Rooney kuivaa Man City kesho

http://cdn.images.express.co.uk/img/dynamic/67/590x/Rooney-Lampard-goals-498076.jpg
Rooney na Lampard
IMETHIBITISHWA kuwa nahodha wa Man United, Wayne Rooney ataanza mechi ya kesho Jumapili dhidi ya Man City katika pambano la watani wa jadi wa jiji la Manchester.
Rooney amemaliza adhabu ya kadi nyekundu na imethibitika kuwa yupo fiti kwa pambano hilo, ingawa mkali mwingine Radamel Falcao hatacheza kwa sasa bado yu majeruhi.
Man Utd ikimkosa Falcon wenzao Man City watakaokuwa nyumbani uwanja wa Etihad watawakosa David Silva, Frank Lampard na Yaya Toure walio majeruhi, lakini samir Nasir atakuwapo dimbani.
Timu hizo zinakutana kesho katika pambano la Ligi Kuu ya England sambamba na mechi nyingine ya Aston Villa dhidi ya Spurs huku matokeo baina yao yakisomeka hivi:
2013-14 - Utd 0-3 City, City 4-1 Utd
2012-13 - Utd 1-2 City, City 2-3 Utd 
2011-12 - City 1-0 Utd, City 2-3 Utd (FA Cup), Utd 1-6 City
2010-11 - City 1-0 Utd (FA Cup), Utd 2-1 City, City 0-0 Utd,
2009-10 - City 0-1 Utd, Utd 3-1 City (FA Cup), City 2-1 Utd (League Cup), Utd 4-3 City

No comments:

Post a Comment