STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 1, 2014

Ndanda yaizamisha Azam, Ruvu yafa Tanga

Azam
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjB-9RKNmxBvoK7JPffvXITg0AN-GJQDTxgjaeWTCCkbeHlJrk8-AQMCg9V_N2hzBqWZPwbFvB1p_5uqtIpEwu-dSq-Dbq5gzX9MHYXEtcYlcJY2X5aPsyLTO1GojedsFeg1g2hj9c06GA/s1600/IMG-20140913-WA0029.jpg
Ndanda Fc
BAO pekee lililofungwa na mchezaji wa zamani wa Toto Africans na African Lyon, Jacob Massawe lilitosha kuipa ushindi wa kwanza Ndanda ikiwa uwanja wake wa nyumbani kwa kuilaza mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam kwa bao 1-0.
Kipigo hicho ni cha pili mfululizo kwa Azam baada ya mechi iliyopita mabingwa hao kufungwa bao 1-0 na JKT Ruvu na kuwaacha 'Matajiri' hao kusalia na pointi zao 10 baada ya kucheza mechi 7.
Ushindi huo umeipa faraja wenyeji Ndanda ambao walikuwa hawajapa ushindi wowote kwenye uwanja wa nyumbani baada ya kufungfwa mechi mbili mfululizo na Ruvu Shooting na Mgambo Fc.
Katika mechi nyingine Prisons-Mbeya ikiwa ugenini mjini Shinyanga ililazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya Stand United.
Prisons walianza kuandika bao mapema kupitia kwa Ibrahim Mamba kabla ya wenyeji kusawazisha kupitia kwa Heri Mohammed.
Nayo timu ya Ruvu Shooting wamejikuta wakizimwa wimbi lake la ushindi baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Coastal Union.
Bao pekee la Wagosi wa Kaya liliwekwa kimiani na Itubu Imbem dakika ya 54,
Stand Utd-Heri Mohammed
Prisons-Ibrajim Mamba

No comments:

Post a Comment