STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 28, 2015

Breaking Newzz: Kapt John Komba hatunaye Duniani

http://api.ning.com/files/8KNI8B2SjT1ePQsfa9AOokVE6RIW8oxFgc*7KyWSQJstmtSfJD-qgiJyCgz83-xe8mTLl34zGqpA5MWQWGNYVtMK4y*tvtqP/1.png?width=650
Kapteni John Komba
 HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba amefariki dunia jioni hii jijini Dar es Salaam.
Taarifa hizo zinasema kuwa Mbunge huyo aliyekuwa pia Mkurugenzi wa kundi la TOT amefariki akiwa hospitalini ya TMJ akipatiwa matibabu.
Kwa mujibu wa taarifa hizo zinasema kuwa, Mbunge huyo alizidiwa akiwa nyumbani kwake Mbezi na kukimbizwa hospitalini hapo akisumbuliwa na ugonjwa wa Kisukari.

MICHARAZO inaendelea kufuatilia taarifa hizo kwa zaidi ili kuwajuza kwa undani zaidi na kujua juu ya taratibu za mazishi ya mwanasiasa huyo aliyekuwa mahiri kwa kuimba Kwaya aliyeanzia Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
Kadhalika MICHARAZO inatoa pole kwa familia, ndugu jamaa na rafiki wa marehemu Kapteni Komba kwa msiba huo mzito ikiwakumbusha kuwa Kila Nafsi itaonja mauti na Kwa hakika sisi ni wa Allah (SW) na Kwake TUTAREJEA. Mungu aiwe roho ya marehemu mahali pema Ameen.

No comments:

Post a Comment