STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 28, 2015

Rooney aibeba Man Utd, Saint's wafa ugenini

3pm banner 10.jpg
Muunganiko wa picha kama zilizochapishwa na Daily Mail zikionyesha Man Utd walipoizamisha Sunderland
MABAO mawili kutoka kwa Mshambuliaji wa kimataifa wa England, Wayne Rooney wameiwezesha Manchester United kupata ushindi nyumbani dhidi ya Sunderland na kufufua matumaini yao ya kuwania nafasi ya ushiriki wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani.
Rooney ambaye kwa muda mrefu amekuwa akichezeshwa kama kiungo na kocha Louis Van Gaal, leo alichezeshwa kama mshambuliaji wa kati na kmufunga mabao hayo katika kipindi cha pili na kuipa Mashetani Wekundu ushindi huoi muhimu.
Nahodha huyo alifunga bao la kuongoza kwa mkwaju wa penati dakika ya 66 kabla ya kuongeza la  pili dakika ya 84 na kupoza machungu na hasira walizokuwa nazo mashabiki wa timu hiyo baada ya wiki iliyopita kulala kwa Swansea City.
Katika mechi ya mapema West Ham United ikiwa nyumbani ilicharazwa mabao 3-1 na Crystal Palace, huku Swansea ikiendeleza ubabe katika ligi hiyo kwa kuilaza Burnley nyumbani kwao kwa bao 1-0 huku Newcastle United ikishinda nyumbani bao 1-0 dhidi ya Aston Villa.
Nayo timu ya Stoke City iliitambia nyumbani Hull City kwa kuilaza bao 1-0 sawa na ilivyokuwa kwa West Bromwich iliyoitambia Southampton waliowafuta kwao.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa mechi mbili za kuakta na mundu, kwa Liverpool kuikaribisha mabingwa watetezi Manchester City na Arsenal kuialika Everton, wakati Chelsea na Tottenh ham Hotspur wenyewe wataumana kwenye mchezo wa fainali za Kombe la Ligi (Capital One)

No comments:

Post a Comment