STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 28, 2015

Classic Mawe, Cheka kumaliza ubishi leo uwanja wa Taifa

Mabondia Mwinyi Mzengela (kushoto) na Shomari Milundi wakitunishiana misuri baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano utakaofanyika leo Uwanja wa ndani wa Taifa
Mabondia Mwinyi Mzengela (kushoto) na Shomari Milundi wakitunishiana misuri baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano utakaofanyika leo Uwanja wa ndani wa Taifa

Bondia Fadhili Majiha akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na Francis Miyeyusho utakaofanyika leo Uwanja wa ndani wa Taifa

Bondia Epson John wa Morogoro (kushoto) akitunishiana misuli na Vicent Mbilinyi baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika uwanja wa ndani wa Taifa katikati ni mratibu Antony Rutta

Bondia Cosmas Cheka (kushoto) akitunishiana misuli na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' baada ya kupima uzito kwa ajili ya pambano lao la ubingwa wa U.B.O Afrika utakaofanyika leo Uwanja wa ndani wa Taifa
Bondia Ibrahim Class akipima uzito kwa ajili ya pambano la UBO Afrika litakalofanyika leo
Bondia Francis Miyeyusho akipima uzito
Bondia Cosmas Cheka (kushoto) akitunishiana misuli na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' baada ya kupima uzito kwa ajili ya pambano lao wa ubingwa wa U.B.O Africa utakaofanyika leo kwenye Uwanja wa ndani wa Taifa jijini Dar es Salaam
BONDIA Ibrahimu Class 'King Class Mawe' amejigamba kumpiga bondia Cosmas Cheka kwenye pambano lao la raundi kumi kugombania ubingwa wa U.B.O Africa utakaofanyika leo katika Uwanja wa ndani wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Ibrahim aliyasema hayo wakati wakipima uzito na afya kwa ajili ya maandalizi ya pambano hilo ambalo limevuta hisia za mashabiki wa ndondi kutokana na ubora wa mabondia wote.
“Namfahamu vizuri Cheka ila nitahakikisha nampiga mapema ili kuhakikishia mashabiki kuwa mimi ni bora kuliko yeye”, alijigamba Ibrahim

Pambano huo utatanguliwa na ngumi kali kutoka kwa bondia Fransic Miyeyusho atakayepigana na Fadhili Majiha pambano la raundi nane.

Pia kutakuwepo na pambano lingine la ubingwa kati ya Alibaba Ramadhani na Jacobo Maganga ambalo litasindikizwa na mapambano makali ya bondia chipukizi, Vicent Mbilinyi ambaye ataoneshana umwamba na Epson John wa Morogoro.

 Naye Shomari Milundi atapambana na Mwinyi Mzengela huku Husein Mbonde atakabiliana na Shedrack Ignas na bondia Said Mundi wa Tanga atapambana na Ramadhani Shauri  pia kutakuwepo mapambano mengine mbalimbali kuhakikisha pambano huo unakuwa wa kihistoria na kuacha gumzo.

Pambano hili linasimamiwa na P.S.T chini ya rais wake Emanuel Mlundwa na mashabiki wamehakikishiwa usalama wa mali zao kwani kutakuwa na ulinzi wa kutosha.

Mabondia Mwinyi Mzengela (kushoto) na Shomari Milundi wakitunishiana misuri baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano utakaofanyika leo Uwanja wa ndani wa Taifa

Bondia Fadhili Majiha akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na Francis Miyeyusho utakaofanyika leo Uwanja wa ndani wa Taifa

Bondia Epson John wa Morogoro (kushoto) akitunishiana misuli na Vicent Mbilinyi baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika uwanja wa ndani wa Taifa katikati ni mratibu Antony Rutta

Bondia Cosmas Cheka (kushoto) akitunishiana misuli na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' baada ya kupima uzito kwa ajili ya pambano lao la ubingwa wa U.B.O Afrika utakaofanyika leo Uwanja wa ndani wa Taifa
Bondia Ibrahim Class akipima uzito kwa ajili ya pambano la UBO Afrika litakalofanyika leo
Bondia Francis Miyeyusho akipima uzito
Bondia Cosmas Cheka (kushoto) akitunishiana misuli na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' baada ya kupima uzito kwa ajili ya pambano lao wa ubingwa wa U.B.O Africa utakaofanyika leo kwenye Uwanja wa ndani wa Taifa jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment