STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 4, 2015

YANGA, COASTAL UNION NI VITA TUPU LEO MKWAKWANI

Wagosi wa Kaya, Coastal Union waliopania kuwatia maumivu vijana wa Jangwani leo Mkwakwani
Yanga waliopa kuondoa 'gundu' Mkwakwani kwa kuinyoa Coastal Union
COASTAL Union wametangaza vita ya dakika 90 dhidi ya Yanga katika mechi pekee ya leo ya Ligi Kuu Tanzania Bara, inayopchezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, huku Yanga wenyewe akitamba kuwa wameenda Mkwakwani kuchukua pointi tatu kwa wenyeji wao.
Timu hizo zinakutana kwenye mchezo nhuo wa kiporo huku kila moja ikitoka kulazimishwa sare isiyo na mabao nyumbani katika mechi zao za mwishoni mwa wiki.
Yanga ilibanwa na Ndanda Fc kwenye uwanja wa Taifa, wakati Coastal ikiwa nyumbani ilishindwa kufurukuta kwa Mtibwa Sugar, hali inatyofanya pambano la leo kuwa kama vita ya kusaka pointi tatu kwa timu zote.
Coastal kupitia Msemaji wake, Oscar Assenga, amesema kuwa kikosi chao kipo tayari kuwatoa nishai Yanga, wakati Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro akisema wameenda Tanga kuchukua pointi tatu kwa vile timu yao ni bora kuliko wapinzani wao.
Coastal inayonolewa na kocha James Nandwa kutoka Kenya itakuwa na kibarua kigumu kwa wapinzani wao licha ya kwamba kwa muda sasa Yanga haijaonja ushindi Mkwakwani dhidi ya Wagosi wa Kaya ama Mgambo JKT.
Mara ya mwisho Yanga kuibuka na ushindi dhidi ya Coastal kwenye Uwanja wa Mkwakwani ilikuwa Novemba 12, 2012 iliposhinda 2-0.
Katibu Mkuu wa Coastal Kassim El Siagi alisema angetaka mashabiki wa soka kuthibitisha ipi timu ya soka la kweli la uwanjani na timu za magazetini ambao namna wanavyopambwa unaweza kusema ni Barcelona ilihali ni timu ya kawaida ionayoshindwa kuzifunga hata timu ndogo kama Ruvu Shooting na Ndanda FC.
Hata hivyo Yanga wameapa kufanya kweli leo baada ya kushuhudia safu yake ya ushambuliaji katika mechi tatu ilizocheza za Ligi Kuu ikifunga moja tu walipoilaza Polisi Moro.
Mashabiki wa Yanga pamoja na timu yao wapo mjini Tanga tangu majuzi kwa ajili ya pambano hilo ambalo litatoa taswira mpya ya msimamo wa Ligi Kuu timu mojawapo ikipata ushindi, Yanga ikiweza kurejea kileleni baada ya kutemeshwa muda mrefu na Mtibwa Sugar na baadaye Azam.
Kadhalika Coastal ikishinda inaweza kukwea hadi nafasi ya pili na kuwaengua Yanga waliopo katika nafasi hiyo kwa sasa wakiwa na pointi 19, mbili nyuma ya Azam wanaoongoza na pointi zao 21.
MSIMAMO LIGI KUU ULIVYO KWA SASA
                             P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Azam              11  06  03  02  15  08  07   21
02.  Yanga            11  05  04  02  12   07  05  19
03. Mtibwa Sugar  11  04  06  01  13  07  06   18
04. Polisi Moro      13  04  06  03   10  09  01  18
05. JKT Ruvu        13  05  03  05   13   13  00  18
06. Ruvu Shooting13  05  03   05   09   10  -1  18
07. Coastal Union 12  04  05   03  10   08  02  17
08. Simba            12  03  07   02   13   11  02  16
09. Mbeya City     12   04  03  05  08   10  -2   15
10. Kagera Sugar 13  03  06  04   10   11   -1  15
11. Mgambo JKT  11  04  02  05   06    10  -4  14
12. Ndanda Fc     13  04  02   07  12    17  -5  14
13. Stand Utd      13  02  05   06   08   16  -8  11
14. Prisons          12  01  07   04   09   11  -2   10

No comments:

Post a Comment