STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 15, 2013

Adebayor aivusha Spurs robo fainali, Chelsea, Newcastle wawafuata



Adebayor akipongezwa na mchezaji mwenzake baada ya kufunga bao jana

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Togo, Emmanuel Adebayor jana aliiwezesha timu yake ya Tottenham Hotspurs kufuzu Robo Fainali ya michuano ya Ligi ndogo ya Ulaya (Europa League) baada ya kufunga bao dakika za nyongeza dhidi ya Inter Milan.
Adebayor ni kama aliwanyamazisha mashabiki wa wenyeji waliomdhihaki katika mechi hiyo kwa kumuiitia ndizi wakimfananisha na nyani kwa kufanya matokeo ya mwisho wa pambano hilio lililochezwa Italia kuisha kwa Inter kushinda 4-1.
Hata hivyo matokeo hayo hayakuiwezesha timu hiyo ya Italia kusonga mbele baada ya kuchezea kichapo cha mabao 3-0 katika mechi ya awali wiki iliyopita na matokeo ya jumla kuwa mabao 4-4.
Spurs ambayo ilimkosa winga wake nyota, Garreth Bale inasonga mbele kwa faida ya bao la ugenini lililofungwa na Adebayor.
Mabao yaliyotishia kuing'oa Spurs kabla ya kwenda muda wa ziada yalifungwa na Cassano dakika ya 20, Palacio dakika ya 52 kabla ya William Gallas kujifunga dakika ya 75 na kufanya dakika 90 mechi hiyo kuisha kwa Inter kushinda mabao 3-0.

Katika muda wa ziada Adebayor aliiandikia Spurs bao dakika ya 96 kabla ya Inter kuchomoa dakika nne baadaye na kufanya hadi dakika ya 120 matokeo kuwa mabao 4-1 Inter wakiibuka kidedea.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo ya Ulaya, Newcastle United ilipata ushindi wa bao 1-0 nyumbani dhidi ya Anzhi Makachkala, Chelsea nayo ikipata ushindi wa mabao 3-1 na kuing'oa Steaua Bucharest.
Mabao ya Chelsea iliyochezea kichapo cha bao 1-0 ugenini yalifungwa na Mata dakika ya 33, John Terry mabao 58 na Fernando Torres dakika ya 71 wakati bao la kufutia machozi la wageni, liliwekwa kimiani na Chiriches aliyefunga dakika ya 45.
Matokeo mengine ya mechi za michuano hiyo iliyochezwa usiku wa jana ni kama ifuatavyo; Lazio iliifunga Stuttgart mabao 3-1 magoli yake yote yakifugwa na Libor Kozak na kufuzu robo fainali kwa jumla ya mabao 5-1, Fenerbahçe ilitoka sare ya 1-1 dhidi ya Victoria Plzen na Fenerbahce kusonga kwa ushindi wa mabao 2-1.
Benfica ilipata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Bordeaux na kufuzu hatua hiyo kwa jumla ya mabao 4-2, huku Rubin Kazan ikisubiri muda wa nyongeza kuing'oa Lavente kwa mabao 2-0 na Zenit licha ya kushinda nyumbani bao 1-0 iling'oka kwa Basel baada ya awali kufungwa mabao 2-0 na hivyo kutoka kwa mabao 2-1.
Kwa matokeo hayo timu zilizotinga hatua hiyo ni hizi zifuatazo:
Newcastle United, Chelsea na Tottenham Hotspurs zote za Uingereza, Lazio ya Italia, Fenernahce ya Uturuki, Benfica ya Ureno, Robin Kazan ya Russia na Fc Basel ya Uswisi.

MISS UTALII TANZANIA WAPONGEZWA


Raisi wa Miss Utalii Tanzania Ndugu Erasto G. Chipungahelo akimkaribisha Mratibu wa masoko wa Chuo kikuu cha Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma kuzungumza na washiriki wa Miss Utalii (hawapo pichani).
Mratibu wa Masoko wa Chuo kikuu cha waandishi wa Habari Bi Sophia akiwakaribisha washiriki wa Miss Utalii Tanzania Taifa 2012/13 Chuoni hapo.
Washiriki wa Miss Utalii Tanzania Taifa 2012/13 wakiwa katika picha ya Pamoja na Mratibu wa Masoko wa Chuo Kikuu cha waandishi wa habari na Mawasiliano.
 
Chuo Kikuu cha Waandishi wa kimewapongeza Miss Utalii Tanzania Taifa 2012/13 kwa elimu walizo nazo na kuwasihi watumie elimu zao kutangaza utalii wa Tanzania Jambo ambalo lina manufaa makubwa kwa jamii ya Watanzania Akizungumza na washiriki hao Kijitonyama Jijini Dar es salaam,
Mratibu wa masoko wa chuo hicho ndugu Sophia Ndibalema aliwataka kutumia Fulsa ya kuwa warembo hasa utalii kwa kujitaftia nafasi zaidi za elimu ya juu kwa manufaa yao Jamii na Taifa kwa ujumla, alisema nafasi zipo wazi kwa wale wenye kuhitaji na wenye sifa za kujiunga chuoni hapo kwa nafasi ya Cheti, Diploma na Shahada, alisema amefurahishwa na muonekano wa asili na mavazi ya heshima kwa washiriki hao hivyo kuondoa dhana kuwa washiriki wa urembo kuwa ni wale wanaovaa mavazi yenye Kudhalilisha jamii hii inathibitisha kuwa Miss Utalii ni Zaidi ya Mashindano Mengine na ni Alama ya Urithi wa Taifa na kielelezo cha mwanamke au Binti wa Kitanzania